DC ILALA ATOA MAAGIZO MAZITO URASIMISHAJI ARDHI
MKUU wa Wilaya ya Ilala, Ng’wilabuzu Ludigija, ameeleza kuchoshwa na malalamiko ya wananchi juu ya kudaiwa kutapeliwa na kampuni zinazohusika na urasmishaji ardhi na kuyataka makampuni yaliyoshindwa kufanya kazi hiyo kujiondoa.
Ameonya, kampuni yoyote ya ardhi iliyopewa kazi hiyo ambayo mmiliki wake atashindwa kuwasilisha taarifa kwa wanachi, kuto kuhudhuria vikao na kuitikia wito atakamatwa na polisi.
Aliyasema hayo Dar es Salam,leo katika kikao kilicho husisha, wakandarasi wa urasimishaji ardhi, wenye viti wa serikali za mitaa, watendaji wa kata na mitaa, maofisa ardhi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na mkoa huo pamoja na wenyeviti wa kamati za urasmishaji ardhi za mitaa.
Ludigija, alisema anasikitishwa na malalamiko mengi anayoendelea kupokea kutoka kwa wananchi juu ya migogoro ya ardhi hasa urasimishaji huo, ambapo wengi wanalalamikia makampuni yaliyopewa kazi hiyo kuchukua fedha na kuingia mitini.
“Nimechoshwa na malalamiko ya migogoro ya ardhi hasa katika urasimishaji. Kama kuna kampuni ambayo ilipewa kazi hiyo na wananchi kupima mitaa yao na inaona imeshindwa kuendelea na urasimishaji ijiondoe ili kazi hiyo ifanywe na watu wengine,”alisema.
Pia mkuu huyo wa wilaya alitaka kampuni zote zillizopewa kazi hiyo kuhuisha mikataba yao ya urasimishaji ardhi waliyosainisha na wananchi kwani mingi imekwisha muda wake.
“Ninatoa siku saba wahusika wote waripoti Juni 13 asubuhi katika kikao kitakachofanyia katika ukumbi wa Arnatoglou kitakacho hususha wadau wote,”alieleza Ludigija.
Alisema yapo makampuni 50 ya urasimishaji ardhi yanayofanya kazi wilayani humo lakini asilimia kubwa yanalalamikiwa na wananchi kwa kushindwa kutekeleza wajibu wao.
Ludigija aliagiza wenye viti wa serikali za mita kuitisha mkikutano ya wananchi katika maeneo yao na kuwapa taarifa sahihi za namna ya zoezi la urasimishaji linavyoendelea.
Alisema, Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan inataka kila kipande cha ardhi kina pimwa, ili wananchi watumie nyumba na ardhi yao kufanya shughuli za maendeleo, ikiwemo kupata mikopo.
Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa wilaya alionya, wananchi ambao hawatarasimisha ardhi kwa makusudi, serikali wilayani humo haitasikiliza migogoro yao inayo husu ardhi na badala yake waende moja kwa moja mahakamani.
“Wapo wanaoona urasimishaji ardhi ni hiyari. Hawatoi fedha za kurasimisha ardhi yao. Tukimaliza urasimishaji huu kama kuna mwananchi atakuwa ameshindwa kurasimisha eneo lake asije ofisini kwangu. Sitashughulikia mgogoro wake,”
Awali, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salam, Tabu Shaibu, alikili kuwepo kwa changamoto za aardhi na kueleza kuwa serikali itashughulikia kikamilifu ili kuhakikisha wananchi wanapata haki yao.
Kaimu Kamishna wa Ardhi Msaidizi wa Mkoa wa Dar es Salam, Idrisa Kayera, alisema ipo changamoto ya elimu ya kutosha kwa wananchi kuhusu urasimishaji ardhi na wengi kushindwa kutoa fedha kwa wakati hivyo kukwami sha kazi hiyo.
Kwa upande wa Katibu wa Makampuni ya Urasimishaji Ardhi Wilayani Ilala, Clemence Mero, alisema changamoto kubwa ni wananchi kuto kulipa fedha, hivyo kampuni nyingi kushindwa kutekeleza wajibu kwa wakati.
“Kwa kweli hali hii imeshusha hata heshima ya kampuni zetu kwa kuitwa matapeli. Wananchi hawatoi fedha za kupiwa ardhi kiasi kwamba tunalazimika kutumia fedha zetu za mifukoni,”alisema.
Kwa upande wa wenye viti wa kamati za urasimishaji ardhi wilayani humo, walisema kila sehemu linapofanyika zoezi hilo kuna vilio vya wananchi kutapeliwa fedha na kampuni husika.
“Hali ni mbaya. Tunaiomba serikali iingilie kati suala hili la urasimishaji. Wananchi hawatuamini tena wenye viti wa kamati. Tunaonekana matapeli. Wamiliki wa kmpuniza urasimishaji hawapokei simu, hawahudhurii vikao na wengine wamefunga ofisi zao na kukimbia,” Alisema Bw George Mtambalike,







