Breaking News

Waziri wa Kigwangala Azindua Muhuri wa Usalama Kutoka Baraza la WTTC

Waziri wa Maliasili na Utalii Khamisi Kigwangala  amezindua rasmi Muhuri wa usalama kutoka Baraza la usafiri na Utalii dunia WTTC uliopokelewa nchini Julai 22 mwaka huu.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa Muhuri huo jijini Dar es salaam, Waziri Kigwangala ameushukuru uongozi wa awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli kwa umahiri ulionekana kwa kuthibiti ugojnwa wa Covid 19, na kupelekea Tanzania kufungua mipaka huku tukichukua hatua madhubuti katika kujinga na ndio sababu kubwa inatufanya leo kuwa hapa na kutumia muhuri wa usalama.

Aidha Kingwangala amempongeza katibu mkuu mpya wa wizara ya maliasili na utalii Aloyce Nziku kwa juhudi walizozifanya katika kipndi chote cha Covid 19, kwa kutokusita kushirikiana na balozi za Tanzania kuifikia dunia na kutangaza utalii wa Nchi.