Breaking News

PROF. MBARAWA AONYA TPA KUPEANA KAZI KINDUGU


 

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa ameitaka Bodi mpya ya usimamizi wa Mamlaka ya Bandari nchini Tanzania (TPA), kuhakikisha inayapatia ufumbuzi matato yanayoikabili mamlaka hiyo kwa hivi sasa.
Prof.Mbarawa ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na bodi hiyo kupitia Teknolijia ya video toka mjini Dodoma na kubainisha kuwa TPA inakabiliwa na matatizo mengi ikiwa ni pamoja na wafanyakazi kupeana ajira kindugu.
Pia Waaziri, alitaja utendaji usiozingatia matokeo, na mifumo mibovu ya ukusanyaji mapato hali inayosababisha utendaji usiozingatia ufanisi.
Kwa upande wake Mwenyekiti mpya wa bodi hiyo Prof. Ignas Rubaratuka amemhakikishia waziri Mbarawa kuwa bodi yake imejipanga kukabiliana na matatizo yote ya bandari nchini ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa weledi mkubwa.
Na shehe semtawa