Breaking News

SALMA JABU (NISHA), KULA FUTARI NA WATOTO WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA HATARISHI DAR





Mwigizaji wa filamu za kitanzania Bi, SALMA  JABU maarufu kama (Nisha) ameandaa futari kwa watoto waishio katika mazingia hatarishi waishio jijini dar es salaam siku ya tarehe 26 mwezi huu.
 
Akizungumza na wandishi wa habari leo juu maandalizi amesema futari imewalenga zaidi watoto wanaoishi katika vituo vya kulelea yatima pamoja na wale ambao wapo mitaani hawana sehem maalum ya kuishi inataji kufanyia katika viwanja vya shule ya sekondari ya Azania jiji da es salaam.

“Katika kuhakikisha watoto wanaishi katika mazingira magumu nao wanashiriki kikamilifu katika mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhan ameona ni vema kuwaandalia futari hili nao wanashiriki vyema katika kipindi chote cha mfungo kama watoto wengine”

Amesema kufata nguzo za dini ya kiislam, kipindi hichi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani, waislam wanapswa kutoa Dhaka pamoja na kuonyesha upendo kwa wengine hususani walio katika mazingira magumu hasa watoto yatima, watoto wenye ulemavu wa ngozi,walemavu pamoja na watu wenye mahitaji maalum hili kuweza kuwafanya wapate faraja kubwa nao.

Aidha msanii huyo bi, SALMA JABU (Nisha) ameongeza kuwa hafla hiyo ya futari inatarajiwa kuzuliwa na  makamu wa rais wa jamhuri wa muungano wa Tanzania mhe SAMIA SULUHU HASANI, Mbunge wa jimbo la Ilala MUSSA ZUNGU,  Mkuu wa mkoa wa dare s salaam PAUL MAKONDA, viongozi wa dini pamoja na wasanii mashuhuri.