NAIBU WAZIRI KIPANGA: SERIKALI INATAMBUA MCHANGO WA WADAU KATIKA KUBORESHA SEKTA YA ELIMU NCHINI
SERIKALI imesema inatambua mchango mkubwa wa Asasi za kiraia
na wadau wa elimu nchini hususani katika kusaidia, kushauri na kuboresha
ya Mitaala ya elimu nchini ili kuwezasha Wahitimu waweze kujiajiri na
kuajiriwa.
Akizungumza wakati akifunga Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa
Elimu Bora (International Quality Education Conference-IQEC) unaandaliwa na
Mtandao wa TEN/MET, uliofanyika jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri wa Elimu
Sayansi na Teknojia Mheshimiwa Juma Kipanga amesema asasi za kiraia zimekuwa na
mchango mkubwa na wadau muhimu hasusani katika kushauri namna bora ya kuboresha
mitaala ya elimu nchini.
“Serikali inatambua na inaunga mkono jihitada za wadau wa
sekta ya elimu nchini katika kuhakikisha kuwa wahitimu wetu wanakidhi soko la
kimataifa na kuweza kujiajili pindi wanapomaliza masomo yao”
Alisema serikali kwa upande wake imeshaanza kuchukua hatua
mbalimbali za kuhakikisha kuwa mpaka kufika Mwaka 2025 kila Mtoto wa Kitanzania
Anapata Elimu Bora na inayokidhi viwango vya soko la ajira.
"Elimu hii Bora inaendana na Uboreshwaji wa Mazingira
Rafiki ya Utatikanaji wa Elimu ikiwemo Miundombinu Wezeshi ya Wanafunzi ambao
Wanamahitaji Maaluum". Alisema Naibu Waziri Juma Kipanga.
Katika hatua nyingine mhe. Kipanga Aliongeza kuwa Ni vyema
wadau wakaendelea kujitokeza kuendelea kutoa maoni yao ambayo yatasaidia kuboresha Mitaala ya Elimu iwe inayoendana na soko la
Ajira la sasa.







