LHRC YAZINDUA RASMI MWEZI WA DEMOKRASIA KUCHANGIZA SIASA ZENYE USHINDANI NCHINI
Akizungumza katika uzinduzi huo jijini Dar es salaam,
Mkurugenzi wa mtendaji wa LHRC, Wakili Anna Henga alisema katika kipindi hicho kituo
kitafanya shughuli mbalimbali za kijamii
ikiwemo utoaji wa elimu juu ya umuhimu wa kuwa na katiba mpya.
“LHRC kimeandaa dodoso maalum la maswali ambalo litakuwa na
maswali muhususi kujua mtizamo wao juu ya katiba mpya, wangependa mchakato huo
uanze na lini wangependa mchakato huo ukamilike ambapo wananchi watatakiwa
kujaza” Alisema wakili Henga
Alisema tayali watanzania zaidi ya 1000 tayali wameshashiriki
kujaza dodoso hilo ambalo linalenga kupata tathimini yao juu ya masuala mbalimbali
hususani upatikanaji wa katiba mpya pamoja na utoaji wa elimu kwa wananchi juu
ya umuhimu wao kushiriki katika maswala ya kidemokrasia.
“LHRC tangu kuanzishwa kwake mwaka 1995 wamekuwa mstari wa
mbele kuijengea jamii yenye kutambua haki na usawa sambamba na kuwajengea
uwezo, kukuza kutetea na kuchangiza mambo yanayohusu haki za binadamu na
utawala bora”
Mwezi wa demokrasia itahitimishwa septemba 15 kwa kufanyika
kongamano kubwa katika ukumbi wa kimataifa wa mwalimu Nyerere ambapo mijadala
juu ya haki za kidemokrasia la mwaka kuu
umebeba kauli mbiu ya “Kuimarisha udhibiti wa demokrasia katika majanga ya siku
zijazo” ikiambatana na maadhimisho ya miaka 30 ya Siasa za ushindani tangu
kurudishwa tena nchi mwaka 1992




