Breaking News

WABUNGE WATEULE BUNGE LA 13 WATUA DODOMA WAANZA KUJISAJILI


Mbunge wa Jimbo la Ilongero mkoani Singida, Haidarali Gulamali akijisajili tayari kwa kushiriki Bunge la 13, litakaloanza rasmi Novemba 11, 2025.

Na Dotto Mwaibale, Dodoma - WABUNGE wateule wa Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamekwisha wasili Dodoma na kuanzia leo Novemba 8 hadi 10, 2025 wameanza kujisajili na kufanya taratibu nyingine za kiutawala, kabla ya kuanza rasmi kwa vikao vya Bunge jipya Jumanne ya Novemba 11, 2025.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Bunge, Baraka Leonard hivi karibuni ilieleza kuwa usajili wa wabunge hao wateule utafanyika katika Ofisi za Bunge, ambapo watafanyiwa zoezi la upigaji picha na uhakiki wa nyaraka mbalimbali.

Moja ya jambo la kwanza litakalofanyika katika kikao cha kwanza cha mkutano wa kwanza wa Bunge la 13 kitahusisha kusomwa kwa tangazo la Rais la kuitisha Bunge, uchaguzi wa Spika, kiapo cha uaminifu kwa wabunge wote, kuthibitisha uteuzi wa Waziri Mkuu, uchaguzi wa Naibu Spika pamoja na ufunguzi rasmi wa Bunge jipya utakaofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wabunge hao wateule wametakiwa kufika wakiwa katika mavazi rasmi na kuwasilisha nyaraka muhimu ikiwemo kitambulisho cha taifa na nakala yake, hati ya kuchaguliwa pamoja na kadi ya benki yenye namba ya akaunti.

Vitu vingine ambavyo vitahitajika ni vyeti vya elimu au taaluma vilivyothibitishwa, cheti cha ndoa kwa walioo au walioolewa, vyeti vya kuzaliwa vya watoto walio chini ya miaka 21 pamoja na wasifu binafsi (CV) wa mbunge husika.

Mbunge wa Jimbo la Babati Mjini mkoani Manyara, Mhe. Emanuel John Kambay akijisajili.

Kazi ya kujisajili ikifanyika.

Wabunge wateule wakijisajili.
Tukio la kujisajili likiendelea.
Wabunge wakijisajili.
Usajili ukiendelea.