Breaking News

DKT. MWINYI AZINDUA AWAMU YA PILI YA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA WA MAMA SAMIA

Na. mwandishi wetu Zanzibar - ‎Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein ‎Ali Mwinyi amezindua Kampeni ya Kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama ‎Samia Awamu ya Pili (MSLAC II).
‎Uzinduzi huo umefanyika leo tarehe 20, Juni 2026 Katika Viwanja vya Dole ‎Kizimbani Wilaya ya Magharibi “A” Mkoa wa Mjini Magharibi ambapo Mhe. Dkt. Mwinyi amezitaka Wizara zote mbili zinazoshughulikia masuala ya sheria kuongeza ushirikiano na kubadilishana uzoefu ili kufanikisha kampeni hiyo.
‎“Kampeni ya Mswaada wa Kisheria ni nguzo muhimu ya kuimarisha Utawala ‎bora, Upatikanaji wa haki na kichocheo cha amani, utatuzi wa migogoro, ‎utulivu na ustawi wa jamii”, akifafanua umuhimu wa kampeni hiyo amesema Dkt. Mwinyi.
Aidha,Mhe. Dkt. Mwinyi kabla ya uzinduzi huo alikagua mabanda ya Maonesho ya ‎Msaada wa Kisheria ambayo ni sehemu ya maadhimisho ya kampeni hiyo na ‎alipata fursa ya kutembelea banda la Idara ya Uhamiaji na kujionea huduma ‎mbali mbali za Masuala ya kiuhamiaji zinazotolewa kwa Umma.
‎Mrakibu wa Uhamiaji Ame Mussa Maulid akimtolea ufafanuzi wa huduma ‎za Uhamiaji Mhe, Rais amesema kuwa Idara ya uhamiaji kupitia maonesho ‎hayo inatoa elimu kwa Umma juu ya huduma mbali mbali zinazotolewa na Uhamiaji Kwa Manufaa ya Taifa.
Akiongeza amesema kuwa wananchi katika Banda la Uhamiaji watapata ‎elimu ya namna ya kuomba pasipoti ya kusafiria, vibali vya ukaazi, viza, hati ‎za dharua za safari pamoja na maombi ya uraia wa Tanzania.
‎Kauli mbiu ya Kampeni ya Kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia ‎inasema “Msaada wa Kisheria kwa Haki, Usawa, Amani na Maendeleo”.