SHIRIKA LA THE FOUNDATION FOR TOMORROW KUENDELEA KUSAPOTI SEKTA YA ELIMU NCHINI
Meneja Program ya mafunzo kwa walimu wa taasisi hiyo, Bwna Noah Kayanda akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu namna shirika hilo linavyoshiki kuwezesha kupatikanaji wa elimu bora.
Dar es salaam:
Shirika la lisilo la kiserikali la The Foundation for Tomorrow litaendelea kushirikiana na serikali katika kuhakikisha inafikia adhama yake ya kuhakikisha inatoa elimu bora na inayokidhi viwango na kwa gharama nafuu kwa wanafunzi wote.
Akizungumza katika kongamano la pili la kimataifa wa masuala
ya elimu bora ulioandaliwa na mtandao wa elimu Tanzania Ten / Met jijini Dar es
salaam, Mkurugenzi wa shirika hilo Bwana Thabisan Ncube amesema shirika wakiwa
kama wadau wa sekta ya elimu nchini wamekuwa wakishirikiana na serikali pamoja
na wadau wengine wa masuala ya elimu nchini kwa kusaidia adhima ya serikali ya
kutoa elimu hususani kwa watoto wanaotoka katika mazingira magumu.
Alisema kupitia programme zao mbalimbali mstari wa mbele
kusaidia na hata kutoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi ikiwemo kuwalipia
ada na mahitaji mengine ya shule kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha sita
kwa lengo la kuwawezesha kufikia malengo yao ya kimaisha na kielimu.
“shirika letu linatambua jitihada za serikali ambazo imekuwa
ikizichukua katika kuhakikisha inaboresha mazingira ya elimu nchini kwa
kutambua hilo tumekuwa tukishiriki katika kuhakikisha adhama hiyo ya serikali
inafikiwa kwa tukitoa scholarship kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu
kuwawezesha kupata elimu bora.” Alisema Bwana Ncube.
Aidha bwana Nembe aliongeza kuwa shirika hilo ambalo makao
makuu yake yapo mkoani Arusha katika miaka 15 tangu kuanzishwa kwake mwaka huu
limeanza kujenga maeneo ya kijamii ya kujifunzia ambayo yatawawezesha wananchi
kujifunza kusoma na kuandika kutoka ndani na nje ya jiji hilo mradi huo upo katika
eneo la Usa river pia utawasaidia wanafunzi wa kitanzania kuendana pia na kasi
ya ukuaji wa kidigitali ili kusaidia katika maendeleo ya Taifa.
Alisema pia taasisi hiyo katika kipindi hicho tayali
imeanzisha mradi wa vituo vya kijamii vya kujifunzia pia watatoa mafunzo ya
ujasiriamali na namna ya kuendesha biashara kwa lengo la kuwapa fursa ya
kuandaa mawazo bora ya kibiashara na jinsi ya kuziendesha hili kuwawezesha kuwainua
kiuchumi
Nae Meneja Program ya mafunzo kwa walimu wa taasisi hiyo,
Bwna Noah Kayanda alibainisha kuwa pia shirika hilo katika kipindi chote cha
miaka 15 tangu kuanzishwa kwake limekuwa likitoa mafunzo kwa viongozi wa shule
katika ngazi mbalimbali ili kuhakikisha kubwa shule zao zinatoa elimu bora.
“Shirika limekuwa likiendesha program mbalimbali katika kipindi hicho tangu kuanzishwa kwake ikiwemo kutoa mafunzo ya kuwajengea uwezo wakuu wa shule za msingi na sekondari kwa lengo la kusaidia seriklai kufikia adhima yake ya kuhakikisha kila mtoto anapata elimu bora na yenye viwango kwa faida yao na taifa kwa ujumla.





